Elimu kama chombo cha ukombozi wa mwanamke katika riwaya ya Nguvu ya Sala
Abstract
Utafiti huu unahusu elimu kama chombo cha ukombozi wa mwanamke katika riwaya Nguvu ya Sala. Usawiri wa mwanamke ambaye ni msomi katika jamii na yule ambaye hajasoma na anavyonyimwa kwa baadhi ya haki. Malengo ya utafiti huu ni Kuchunguza nafasi ya mwanamke msomi anavyopigania haki katika riwaya Nguvu ya Sala na la pili ni Kubainisha mchango wa mwanamke msomi katika ujenzi wa jamii katika riwaya Nguvu ya Sala. Utafiti huu unatathimini ni kiwango gani mwanamke anavyochangia kupigania haki zake baada ya kupata elimu. Ili kufikia malengo ya utafiti huu, Wanawake wanapaswa kufanya kazi pamoja, kama shirika moja linalopigania jingine kama inavyoonyeshwa katika riwaya Nguvu ya Sala.