Ufaafu wa Istilahi za Kiswahili katika Vitabu Rasmi vya NCDC kwa Mtaala Mpya wa Umilisi nchini Uganda
Abstract
Utafiti huu unachunguza ufaafu wa istilahi za Kiswahili zinazotumika katika vitabu vya mtaala mpya wa umilisi wa shule za sekondari nchini Uganda ukizingatia vigezo vya PEGITOSCA na kanuni nyingine za usanifishaji wa istilahi za Kiswahili. Utafiti ulipima istilahi 50 kutoka vitabu rasmi vya NCDC (2020) ili kubaini ubora wake katika matumizi ya kielimu. Matokeo yalionyesha kuwa 70% ya istilahi ni faafu, ingawa changamoto kuu zilibainika katika umataifa, uangavu, na uchumi wa lugha. Mahojiano na walimu yalionyesha kuwa istilahi nyingi ni ndefu, ngumu kueleweka, na hazilingani na lugha ya mawasiliano darasani. Utafiti unahitimisha kuwa mfumo wa istilahi za Kiswahili katika mtaala wa NCDC una msingi thabiti wa kilugha, lakini unahitaji maboresho ya kimkakati ili kuongeza uwazi, urahisi wa matumizi, na mashiko ya kimataifa katika elimu ya sekondari.