dc.description.abstract | Awali ya yote anayestahiki kushukuriwa ni Mwenyezi, Mungu kwa kuniumba, kunikuza na kunipa afya nzuri, uvumilivu, busara na hekima ya kufanya kazi hii hadi kuimaliza. NamwombaMungu anijalie ziada za kheri.
Pili, shukrani zangu zisizo na kikomo ziwafikie wazazi na walezi wangu wapenzi: Bw. Nathan Rwadada na Bi. Molly Kabakanye Rwadada kwa kunizaa na kutochoka kunilea, kunishauri, kunisomesha bila ya kuchoka mpaka sasa. Pia na wale wazazi wamenilea kama Bw. Bashaija Godfrey na Bi. Molly Bashaija, dada zangu Bi. Merab Aryatusasira, Anita Atwiine, Angella, Estella, Eureka, Ada, kaka zangu kwa msaada wenu. Nawaombea Mungu Muumba awajalie mema na baraka zake zisizo na mwisho.
Tatu, shukrani zangu zimfikie Mwalimuwa wangu Dkt. Masengo Innocent, ambaye amekuwa msaada wa kiongozi na mshauri katika matini ya kozi hii ya Utafiti. Bw. Kyomuhendo Victor kwa usaidizi na Usahihishi wake bila kuchoka ili nifanye kazi hii. Sio tu kunisaidia kufaulu Utafiti huu bali pia kunifanya nijifunze na kuelewa kiswahili na shina lake la fonolojia.
Ameniongoza ili niweze kukamilisha kazi kwa wakati mwafaka. Mungu amlipe mema na aishi daima. Shukrani zangu za pekee ziufikie uongozi wa Chuo Kikuu Makerere kwa kunipa fursa hii ya kusoma. Chuo ni kikubwa siwezi kutambua kila mtu lakini ebu nitaje tu wahadhiri wangu: Dkt.Masengo Innocent, Dkt. Mutungi Boaz, Dkt. Asiimwe Caroline, Dkt. Jjingo Caesar, Dkt Masereka Levi Kahaika, Bw. Wambete Francis, Bw. Nsereko Nelson na wengineo na uongozi wa Shule ya Ualimu. Hawa wote juhudi zao kutoka mwaka wa kwanza hadi huu wa mwisho wamekuwa ni dira ya kufanikisha. Walitumia muda wao na rasilimali kunifundisha na siwezi kuchukua juhudi zako ili kuangaza maisha yangu ya baadaye kwa urahisi.
Na walimu wangu wote kutoka shule za msingi hadi shule za upili kama Bi Rolla Atamba aliyenisaidia kupita Kiswahili; pia marafiki zangu wote katika Chuo Kikuu cha Makerere, kama Malangahe Bernadet, Monick, Ronah, Sophie, Shakira, Anthony, Enos, Crispus, miongoni mwa wale wote ambao wamenisaidia kupitisha safari yangu ya elimu Chuoni. Sikuweza kujisimamia mwenyewe na nikafaulu. Mungu awabarikie sana. | en_US |