dc.description.abstract | Utafiti huu unachunguza athari za Kifonolojia za Kinyankore Katika Kujifunza Lugha ya Kiswahili, mintarafu stadi ya kusoma nchini Uganda hasa kwenye shule za upili. Utafiti huu unatumia nadharia ya Fonolojia ili kuweka baina athari hizo.
Katika utafiti huu nimewasilisha na kuchambua na nimekuskusanya data kutoka kwa wanafunzi wenzangu ambao ni wazungumzaji wa lugha ya kinyankore, nimeandika maneno na kuwauliza jinsi wanavyoyasoma kwa kiswahili na nikagundua kuwa kuna baadhi ya fonimu zinatamkwa vibaya na hii ni kwa sababu ya lugha ya mama.
Nitaelezea aina za fonimu za Kinyankore na athari za Lugha ya Kinyankore katika Kujifunza Lugha ya Kiswahili katika mantarafu shule za upili. Sio tu kiswahili ambayo huathiriwa na lugha mama jinsi utafiti huu unavyosisitiza lakini katika hali yoyote ambapo kuna ujifunzaji wa lugha ya pili, lugha ya kwanza inabidi kuingilia ufundishaji na ujifunzaji wa lugha hiyo. | en_US |