Uhusiano wa kimuundo katika mashairi ya kiswahili na ya kinyankole na utenda kazi wake katika ujifunzaji wa kiswahili.
Abstract
Lengo kuu la utafiti huu lilikuwa kuchunguza uhusiano wa kimuundo katika mashairi ya Kiswahili na ya Kinyankore na utendajikazi wake katika ujifunzaji wa Kiswahili. Malengo Mahsusi ni Kubaini muundo wa mashairi ya lugha ya Kiswahili na lugha ya Kinyankore na utenda kazi wake katika ujifunzaji wa kiswahili.kueleza jinsi uhusiano kati ya ushairi wa kiswahili unavyotatiza ujifunzaji wa Kiswahili, kupendekeza njia za kukubaliana na utata wa utenda kazi unaoshababishwa na uhusiano wa muundo wa mashairi ya kiswahili na kinyankole. Utafiti huu uliongozwa na nadharia ya Umuundo iliyowekewa msingi na mawazo ya mwanaisimu Mswizi Ferdinand De Saussure (1909) ambayo yalikitwa katika lugha. Utafiti huu wa nyanjani na maktabani ulifanyiwa katika wilayani Sheema. Mtafiti alitumia eneo la Sheema kwa sababu kuna Wanyankore wengi ambao walimsaidia kupata taarifa juu ya mashairi ya Kinyankore. Mtafiti aliwahoji Wanyankore kumi na wawili wa aina na umri tofauti tofauti yaani wazee na vijana kuhusu mashairi ya Kinyankore. Kwa upande mwingine, mtafiti alitumia maktaba ya Chuo Kikuu cha Makerere kwa kuwa kuna vitabu mbalimbali kuhusu mashairi ya lugha hizo mbili tofauti vilivyotoa taarifa inayohitajika kuimarisha lengo lake la utafiti. Data za msingi zilikusanywa kutoka katika mashairi ya Wanyankore na yale ya Waswahili. Data hizi zilitumika kujaza pengo la utafiti lililoachwa na watafiti tangulizi. Mtafiti alitumia mbinu kadhaa katika ukusanyaji wa data za utafiti huu ili kukamilisha malengo ya utafiti wake kama vile; mbinu ya mapitio ya maandishi, mbinu ya hojaji kati ya nyingine. Matokeo ya utafiti yalionyesha kwamba mashairi ya kiswahili yanaweza kufundishwa vizuri kwa kutumia mbinu kadhaa kwa mfano mbinu ya uigizaji ,ukariri na uimbaji kati ya nyingine.Utafiti huu ulikamilika kwa kutoa hitimisho na mapendekezo yatakayowaongoza watafiti wengine watakaofanya mada yenye uhusiano na hii.