Athari za lugha ya Kitagwenda katika kujifunza matamshi ya lugha ya Kiswahili
Abstract
Lengo kuu la utafiti huu ni kujua jinsi ambavyo mzungumzaji wa lugha ya Kitagwenda anayejifunza lugha ya kiswahili anavyoathiriwa na lugha yake mama katika mchakato mzima wa kujifunza lugha ya kiswahili sanifu. Utafiti huu umefanywa katika Wilayani Kitagwenda. Utafiti huu ulitumia mbinu ya Usomaji na uandikaji matini, Dodoso na mbinu ya kimaktabani katika kukusanya data .
Matokeo ya utafiti huu yalibaini kwamba pana Athari ya Lugha ya Kitagwenda katika kujifunza Lugha ya Kiswahili Sanifu. Hili lilitokana na sababu ya Wazungumzaji wa lugha ya Kitagwenda wanaojifunza lugha ya Kiswahili kuhamisha uelewa wa Lugha ya Kwanza ya Kitagwenda kwenda Lugha ya Pili ambayo ni lugha ya Kiswahili.
Mapendekezo ya Mtafiti ni kwamba lugha ya kijita inaleta athari kwa Wazungumzaji wa lugha ya Kitagwenda wanaojifunza lugha ya kiswahili na wanapokuwa wanajifunza lugha ya kiswahili sanifu. Kuwazuia wanafunzai kuongea lugha ya Kitagwenda katika mzingira ya shuleni, kuweka mkazo katika ufundishaji kwa kutumia lugha hiyo hiyo ili wasiwe na mazoea ya kuongea lugha ya Kitagwenda wakati wa ufundishaji. Kufundisha watoto lugha ya Kiswahili wakiwa wadogo kwa madarasa ya shule za msing kabla ya kukutana nacho shule za sekondari kama ilivyo hapa nchini uganda. Hivi ni kwa sababu lugha ya Kiswahili Nchini Uganda huanzia shule za sekondari ingawa siku hizi serikali inafanya jitihada za kukianzisha shule za Msingi. Walimu wasitumie lugha mama zao wakati wa kuwasiliana na wanafunzi wao darasani au nje ya darasa, hii itawajangea wanafunzi uzoefu na uwezo wa kuwasiliana wao kwa wao watakapokuwa shuleni na pia watakapokuwa nje ya shule kwa lugha ya Kiswahili Sanifu.