Usawiri wa mwanamke kama mvumilivu kwa kurejelea riwaya ya Nyota ya Rehema na Baraka za mama
Abstract
Tasnifu hii inahusu swala la mwanamke kama mvumilivu kwa kulejelea riwaya ya nyota ya rehema na baraka za mama. Madhumuni ya utafiti huu yalikuwa kudadisi mwnamke kama mvumilivu katika riwaya za kiswahili, kwa kuonyesha jinsi mwanamke anavyovumilia katika hali mbalimbali za maisha yakek,kwa mfano katika ndoa, familia, ulezi wa mama wakambo,utabaka nakadhalika, na kuchunguza aina tofauti tofauti za uvumilivu katika riwaya hizi mbili, na pia kuonyesha mifano wanayo tumia hao wanawake kuwa wavumilivukatika riwaya ya Nyota ya Rehema na Baraka za Mama. Katika utafiti huu, mtafiti aliongozwa na nadharia ya ufeminist wa kiafrika na nadharia ya umax, ambayo zilitongozwa katikauchambuzi na uwashilishaji wa data kwakuzingatia mihimili ya nadhalia hizi mbili.Nadharia ya ufeministi wa kiafrika ilifaa utafiti huu kwasababu inashigulikia masuala ya jinsia ya kike na nadharia ya umax lilifaa utafiti huu, kwasababu ina mihimili anbayo inahusiana na swala la wanawake kwa mfano utabaka. Utafiti huu ulijikita katika maktabani ili kupata maandishi yanayohusiana na mada iliyoshugulikiwa. kutokana na maelezo haya, kundi lengwa la utafiti huu ni usawiri wa mwanamke kama mvumilivu. Sampuli iliyotumika ni sampuli lengwaa mbayo ilimusaidia mtafiti kupata data znazohitaji. Utafiti huu ulitumia mbinu ya kusoma na kuandika katika kukusanya data yake. Matokeo ya utafiti yalijitokeza wazi kuwa nafsi ya mwanamke ni kuwamlezi wawatoto,kutii mumewi,kumusaidia mumewe na kudimisha imani ya ndoa. Ukusanyaji na uchanganuzi wa data,uwashilishaji wa matokeo ulifanywa kwanjia ya maelezo katika riwaya ya baraka za mama na riwaya ya nyota ya rehema. Utafiti huu utawafaa watafiti wengine watakaojishughulisha na mada inayohusu mwanamke yani wataweza kulejelea kazi hii ili kupata habari inayohusu nafasi ya mwanamke. Kwa ujumula, utafiti uliyofanywa ulichunguza usawiri wa mwanamke kama mvumilivu kwakulejelea riwaya ya nyota ya rehema na baraka za mama.