Mchango wa wanawake wa kuleta ukombozi katika tamthilia ya Kigogo na Kimya kimya kimya
Abstract
Tafiti nyingi za fasihi ya Kiswahili zimemhusu mhusika mwanamke kwa ujumla. Kipyegon (2013) katika tasnifu yake, "Nafasi na utambulisho wa mwanamke katika Natala na Kifo Kisimani", amesawiri mwanamke akinyanyaswa katika anavyochukiwa katika jamii. Licha ya hayo, juhudi za mwanamke za kujikomboa na kupata hadhi katika jamii zimeangazia. Aidha tafiti chache kama vile za Kimani (2003), Wegesa (1994), Lugano (1985 na 1998) miongoni mwa wengine zimeonyesha kuwa mwanamke amedharauliwa kwa kupigwa, kutawishwa, kutukanwa, kubakwa na kadhalika. Dhuluma hizi zimewaathari wanawake kwa njia mbalimbali kama vile ndoa zao kuvunjika, kukumbwa na upweke na kuasi. Kwa hivyo utafiti huu ulichochewa kuchunguza na kufafanua juhudi za wanawake katika kupigania ukombozi na changamoto wanazokutana nazo. Pia, kubainisha vichochezi vinavyowasukuma wanawake katika mchakato huu mzima.